Viongozi
wa Mataifa ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki wakiimba Wimbo wa Mataifa
hayo kabla ya kuanza kwa Mkutano wao wa 11 kwenye Hoteli ya Ngurdoto
Mkoani Arusha. Kutoka Kushoto kuelekea kulia ni Waziri
Mkuu wa Rwanda Bw. Pierre Damien Habumuryemi, Rais wa Burundi Bw. Pierre
Nkurunziza, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Rais Yoweri Kaguta Museveni wa
Uganda, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho
Kikwete, Rais Uhuru Kenyata wa Kenya na Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyemuwakilisha Rais wa Zanzibar Dkt. Ali
Mohammed Sheni.
Rais
Uhuru Kenyata wa Jamuhuri ya Watu wa Kenya akihutubia Mkutano wa Wakuu
wa Mataifa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mara ya kwanza baada ya
Kuchaguliwa kuwa rais wa Kenya hivi Karibuni.
Baadhi
ya Mawaziri wa SMT na SMZ walioshiriki Mkutano wa Wakuu wa Mataifa ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki kwenye Hoteli ya Ngurdogo Mkoani Arusha
Tanzania. Kutoka kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais MBM Dkt.
Mwinyihaji Makame, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais wa
Zanzibar Mh. Fatma Abdullhabib Fejeji, Waziri wa Afrika Mashariki Mh.
Samuel Sita na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Tanzania Mh. Mahadhi Juma.
Mwenyekiti
wa Mataifa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Yoweri Kaguta Museveni
aliyeshika Kofia akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wenzake wa
jumuiya hiyo mara baada ya kumaliza Mkutano wao wa 11 wa Jumuiya hiyo
uliofanyika Ngurdoto Mkoani Arusha. Kushoto kwa Rais Museveni ni Rais
Jakaya Kikwete wa Tanzania, Rais Uhuru Kenyata wa Kenya na Makamu wa
Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyemuwakilisha Rais wa
Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Sheni. Kulia kwa Rais Museveni ni Waziri Mkuu
wa Rwanda Bw. Pierre Damien Habumuryemi pamoja na Rais wa Burundi Bw.
Pierre Nkurunziza.




No comments:
Post a Comment