ZIARA YA NAPE MOSHI MKOANI KILIMANJARO
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, akipokea kadi ya aliyekuwa mwanachama wa Chadema, kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi, Juma Kalendo, baada ya kutangaza kuhamia CCM, wakati wa mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika Aprili 6, 2013, kwenye Viwanja vya Reli, Kata ya Njoro, Moshi mkoani Kilimanajro. Katika mkutano huo zaidi ya vijana 65 walitangaza kuhamia CCM kutoka Chadema na Nape ametangaza kuwakabidhi kadi za CCM katika hafla maalum itakayoandaliwa baadaye. Kushoto ni Katibu wa CCM mkoa wa Kilimanajro Steven Kazidi. (Picha na Bashir Nkoromo).
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisisitiza jambo wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika Aprili 6, 2013 kwenye Viwanja vya Reli, Njoro mkoani Kilimanajro. (Picha na Bashir Nkoromo).
No comments:
Post a Comment