Saturday, 25 May 2013

RAIS KIKWETE AWASILI ETHIOPIATAYARI KUUDHURIA SHEREHE ZA MIAKA 50 YA UMOJA WA AFRIKA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na maafisa wa ubalozi pamoja na wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa mara alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole jijini Addis Ababa, Ethiopia, Ijumaa Mei 24, 2013 usiku tayari kuungana na viongozi wenzie wa Afrika pamoja na wageni waalikwa katika sherehe za miaka 50 toka umoja wa Afrika (OAU na AU)  kuanzishwa pamoja na mkutano wa kawaida wa umoja huo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakisikilia maelezo toka kwa Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia Profesa Joram Biswalo maara baada ya kuwasili  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole jijini Addis Ababa, Ethiopia, Ijumaa Mei 24, 2013 usiku tayari kuungana na viongozi wenzie wa Afrika pamoja na wageni waalikwa katika sherehe za miaka 50 toka umoja wa Afrika (OAU na AU)  kuanzishwa pamoja na mkutano wa kawaida wa umoja huo
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole jijini Addis Ababa, Ethiopia, Ijumaa Mei 24, 2013 usiku tayari kuungana na viongozi wenzie wa Afrika pamoja na wageni waalikwa katika sherehe za miaka 50 toka umoja wa Afrika (OAU na AU)  kuanzishwa pamoja na mkutano wa kawaida wa umoja huo

RAIS Jakaya Kikwete ni miongoni mwa wageni mashuhuri na marais wa Afrika waliowasili mjini Addis Ababa Ethiopia kwa sherehe za kuadhimisha miaka hamsini tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika leo.
Kauli mbiu ya sherehe za leo ni mjadala mkuu kuhusu ushirikiano wa nchi za Afrika na kuimarishwa kwa muungano huo.

Mwenyekiti wa tume ya muungano huo, Dk Nkosazana Dlamini Zuma, anasema leo itakuwa ni siku ya fursa ya kipekee kwa AU kujadili kuhusu uwezo wa bara hili na ambacho kinaweza kufikiwa katika miaka hamsini ijayo.
Sherehe za AU zinafanyika huku Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto pamoja na mtangazaji wa redio Joshua Arap wakiwa za ghasia za baada ya uchaguzi wa Kenya mwaka 2007/08 katika mahakama ya kimataifa ya ICC.
Duru zinasema kuwa huenda mawaziri wa mambo ya kigeni wa nchi za Afrika wamekubaliana kuhusu azimio linalotaka kesi ya washukiwa hao kurejeshwa Kenya ambako inaweza kusikilizwa na hatua kuchukuliwa dhidi ya watakaopatwa na makosa.
Shereha hizi pia zinakuja wakati bara la Afrika linashuhudia migogoro nchini Mali, DRCongo huku Misri ikiwa bado haijatengamaa baada ya kufanyika mapinduzi ya kiraia yaliyomng'oa mamlakani rais Hosni Mubarak.
Lakini mwenyekiti wa AU ana matumaini kuwa Afrika iko kwenye mkondo mzuri wa kimaendeleo.
Katika hotuba yake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 21 wa AU, Dlamini Zuma alisema kuwa Afrika imekuwa kiuchumi katika muongo mmoja uliopita, imeshuhudia maendeleo ya kiuchumi , ustawi wa kikanda , uimarishwaji wa miundo mbinu na ushirikiano wa kikanda.
Sherehe hizi ambazo zitafuatwa na mkutano wa siku mbili wa marais wa AU, zitatoa fursa kwa wananchi wa bara la Afrika kuangazia ufanisi wa Muungano huo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...