Saturday, 18 May 2013

Teknolojia ya kisasa ya mawasiliano ndiyo mkombozi wa uchumi mataifa machanga - Balozi Seif

 Makamu wa Rais wa Kampuni ya Kimataifa ya Vifaa vya Mtandao wa Teknolojia ya Kisasa ya Zhong Xing Telecommunication Equipment { ZTE }ya Nchini China Bwana Chen Jinsong akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa ZXanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Kulia yao ni Mwakilishi wa Kampuni hiyo Nchini Tanzania ambayo ndio inayosimamia ujenzi wa Mkongo wa Taifa Zanzibar Bwanan Wayne Zhu.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akibadilishana mawazo na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Kimataifa ya Vifaa vya Mtandao wa Teknolojia ya Kisasa ya Zhong Xing Telecommunication Equipment { ZTE } ya Nchini China Bwana Chen Jinsong.
 Mwenyekiti wa Kampuni inayoendesha Miradi ya Hoteli za Kimataifa Afrika Mashariki iitwayo Mada Hotels yenye Makao Makuu yake Mjini Nairobi Nchini Kenya Bwana Tinu Mhajan akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akielezea fursa za uwekezaji zilizopo Zanzibar katika sekta ya Utalii mbele ya Mwenyekiti wa Kampuni inayoendesha Miradi ya Hoteli za Kimataifa Afrika Mashariki iitwayo Mada Hotels yenye Makao Makuu yake Mjini Nairobi Nchini Kenya Bwana Tinu Mhajan
Mwenyekiti huyo wa Mada Hotels alifika Zanzibar kuangalia maeneo ambayo Kampuni yake inaweza kuwekeza katika ujenzi wa Hoteli za Kitalii.
Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...