Monday, 3 June 2013

Kampeni za uchanguzi wa nafasi ya udiwani kata ya Iseke tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi katika picha.

E83A0182
Mjumbe wa halmashauri kuu CCM taifa na waziri katika ofisi ya rais sera na mahusiano, Mh.Steven Wasira (kushoto) akiteta jambo na mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ikungi,Hassan Tati wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni za CCM katika uchaguzi wa udiwani kata ya Iseke.
E83A0183
Mjumbe wa halmashauri kuu CCM wilaya ya Ikungi, Jonathan Njau (wa kwanza kushoto)  akifuatilia kwa makini maendeleo ya uzinduzi wa kampeni za CCM za uchaguzi wa nafasi ya udiwani kata ya Iseke.Wa pili kushoto ni MNEC wa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza, Lawrence Masha, mbunge wa jimbo la Kibaha, Mudi Ijumaa na mbunge wa jimbo la Tarime mkoani Musoma, Nyagwana Nyambiri.
E83A0193
Mjumbe wa halmashauri kuu CCM taifa na waziri katika ofisi ya rais sera na mahusiano, Mh. Steven Wasira (kushoto) akikabidhiwa kadi 350 za CHADEMA na aliyekuwa katibu kata wa chama hicho kikubwa cha upinzani, Francis Antoni.
 E83A0197
Mjumbe wa halmashauri kuu CCM taifa na waziri katika ofisi ya rais sera na mahusiano, Mh. Steven Wasira akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni za nafasi ya udiwani kata ya Iseke wilaya ya Ikungi.
E83A0212
Mjumbe wa halmashauri kuu CCM na waziri katika ofisi ya rais sera na mahusiano, Mh. Steven Wasira (kushoto) akimnadi mgombea wa CCM Amosi Mughenyi anayewania  nafasi ya udiwani kata ya Iseke.
E83A0167
Mjumbe wa halmashauri kuu CCM taifa na waziri katika ofisi ya rais sera na mahusiano, Mh. Steven Wasira,akizindua tawi la CCM kijiji cha Unyangwe.
E83A0188
MNEC (CCM)  wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Jonathan Njau (mwenye shati kijani) akishiriki kikamilifu kutoa burudani na kikundi cha uhamasishaji cha kijiji cha Unywagwe kwenye mkutano wa kampeni za kuwania udiwani kata ya Iseke.(Picha na Nathaniel Limu).

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...