Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Morogoro Innocent Kalogeris kulia akionyesha moja kadi ya Chadema mara baada ya Mwenyekiti wa chama hicho wilaya ya Morogoro kuhamia CCM wakati wa mkutano wa hadhara wa kutathimini ilani ya CCM kwa mwaka 2012/2015 uliofanyika kwenye uwanja wa Shujaa kata ya Mjipya mkoani hapa.
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Morogoro Innocent Kalogeris akizungumza jambo wakati wa mkutano huo wa hadhara wa kutathimini ilani ya CCM kwa mwaka 2012/2015.
Mwenyekiti wa Ulinzi na Usalam mkoa wa Morogoro pia mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera naye akihutumia mkutano huo.
Mbunge wa jimbo la Morogoro mjini Abdullaziz Abood akiteta jambo na Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Morogoro Innocent Kalogeris katika mkutano huo.
Mbunge wa jimbo la Morogoro mjini Abdullaziz Abood ambaye pia ni Mjumbe wa NEC wilaya ya Morooro naye akizungumza katika mkutano huo ambapo ulitoa fursa ya viongozi kueleza majukumu mbalimbali waliyofanya ndani ya chama hicho.
Abel Luanda aliyekuwa Katibu wa chadema mkoa wa Morogoro kushoto na wanachama wengine wa vyma vya upinzani akizungumza jambo mara baada ya kurejesha kadi za vyama vyao ikiwemo Chadema kwa Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi mkoa wa Morogoro Innocent Kalogeris kulia.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Juma Nondo akielezea jambo umati uliohudhuria mkutano huo kazi zilizofanywa na Halmashauri chini ya usimamizi wake akishirikia na baraza la madiwani.
Mwenyekiti wa CCM mkoa huo Mhe, Kalogeris akiteta jambo na Katibu wa CCM mkoa, Sixtus Mapunda katikati na Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joelb Bendera kulia wakati wa mkutano huo.
Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Morogoro Fikiri Juma kulia akiwaeleza jambo wabunge wa jimbo la Morogoro mjini Abdulllaziz Abood kushoto na Dkt Lucy Nkya katikati wa jimbo la Morogoro kushini mashariki wakati wa mkutano huo.
Sehemu ya wananchama wa chama hicho
No comments:
Post a Comment