Thursday, 25 April 2013

RAIS DKT KIKWETE AONGOZA HARAMBEEE YA KUCHANGIA JIMBO LA UKONGA

Rais Dkt. Jakaya Kikwete  akitoa hotuba wakati wa harambee ya kutunisha mfuko wa kuwasaidia wajasiliamali wadogo na wananchi wanaoishi Jimbo la Ukonga kuwainua kimaendeleo.
Bendi ya muziki, The Babloom Trio ikitoa burudani wakati wa kuchangia mfuko wa kuwasaidia wajasiriamali wadogo na wananchi wanaoishi Jimbo la Ukonga kuwainua kimaendeleo. kushoto Mkurugenzi wa bendi hiyo Bw.Seif Kisauji pamoja na wanamziki wengine. SONY DSC 
Rais Dkt. Jakaya Kikwete  akimsikiliza Mbunge wa jimbo la Ukonga Mhe.Eugen Mwaiposa wakati akitoa hotuba yake( wapili kushoto kwake) Mwenyekiti wa Ukonga SACCOS Bi.Adivela Ruge  akitoa hotuba wakati wa harambee ya kutunisha mfuko wa kuwasaidia wajasiliamali wadogo na wananchi wanaoishi Jimbo la Ukonga kuwainua kimaendeleo.
SONY DSC 
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye harambee hiyo SONY DSC 
Isaya Lyimo kutoka CRDB akipewa mkono wa pongezi na Mhe.RAIS Jakaya Kikwete. SONY DSC 
Rais Jakaya Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na wakikundi wa Ukonga SACCOS SONY DSC 
Diwani kata ya Kipawa Mhe Bonnah Kaluwaa (katikat)kiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wake. (PICHA ZOTE NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)
RAIS Jakaya Kikwete ameongoza harambee ya kutunisha mfuko wa kuwasaidia wajasiriamali wadogo na wananchi wanaoishi Jimbo la Ukonga jijini Dar es salaam kuwainua kimaendeleo.
 Katika harambee hiyo iliyofanyika jana kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam na kuudhuriwa na wafanyabiashara mbalimbali kutoka Wilaya ya Ilala, jumla ya sh. mil 462 zilikusanywa ikiwa ahadi na fedha taslimu huku Rais Kikwete akichangia mil 5.
Rais Kikwete akizungumza katika harambee hiyo alitoa pongezi kwa mbunge wa jimbo hilo Eugen Mwaiposa kwa kuandaa mkakati huo ambao kama utasimamiwa vema utasaidia kuinua vipato vya wafanyabiashara wa wadogo na wananchi wenye hali duni ya kuendesha maisha yao.

 Moja ya lengo la harambee hiyo ni kuanzisha SACCOS ambayo itatumika na wafanyabishara wadogo sanjari na wananchi kukopa na kutunisha mitaji yao ya biashara ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
 ”Nimefurahishwa na malengo ya kufanya harambee ili kupata fedha zitakazosaidia kuanzisha SACCOS ambayo ni moja ya Ilani yetu, lakini pia nimejisikia faraja zaidi kuniambia mkakati wenu mwingine ni kuifanya kuwa benki ya Wananchi,”.Alisema Kikwete.
Aliongeza kuwa Serikali haina uwezo wa kuajiri kila mtu katika fani mbalimbali huku akisisitiza kuwa ajira nyingi zinazopatikana Serikalini ni walimu na madaktari lakini kwa sekta nyingine hakuna nafasi za kutosha.
 Hivyo alitoa mwito kwa vyuo vya ufundi Stadi kutoa mafunzo yanayohitajika kwenye soko la ajira ambayo pia yatakayotoa fursa kwa vijana kujiajiri wenyewena kuwaajiri wenzao sanjari na kuwataka vijana kuhakikisha wanachukua mafunzo yatakayowatia ajira kwa uraisi.
Mbunge wa Jimbo hilo, Mwaiposa alisema eneo lake wakazi asilimia 92 ni wajasiriamali wadogo ambao baadhi yao wamo katika nyanja ya Ufugaji na biashara nyingine na wameshindwa kufikia mafanikio kutokana na kuwa na mitaji midogo.
 Aliongeza kuwa harambee hiyo ina malengo matatu moja likiwa ni kuwaondolea changamoto zinazowakabili kwa kuanzisha Saccos na kuendeleza Vikoba 54 vilivyopo sasa kati ya 104 vilivyopo awali.
 Pili alisema kuwa ni kutoa elimu ya biashara na kutafuta masoko hali ambayo itasidia kufikia malengo katika shughuli zao za ujasiliamali sanjari na kuondoa matatizo ya maji ambayo ni kero kubwa kwa wananchi wa huko.
Kabla ya harambee hiyo iliyofanyika juzi, Jimbo hilo lilikuwa na mtaji wa mil. 26 zilizotokana na vikundi 128 vya vikoba na mahitaji yalikuwa ni kupatikana Sh. mil 600.
Licha ya Rais Kikwete kufanya jitihada kubwa ya kuchangisha fedha zilizopatikana wengine waliochangia ni Mkurugenzi Mkuu wa Jambo Concept, Juma Pinto ambaye alitajwa kuchangia Sh. mil 4 japo hakuwepo katika halfa hiyo na kupongezwa na mkuu huyo wa nchi.
 ”Namshukuru Pinto kwa mchango wake wa kuchangia maendeleo ya jimbo la Ukonga na aendelee kuwa na moyo huo ili kukoa vijana katika dimbwi la ukosefu wa ajira”alisema Kikwete.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...