Saturday, 11 May 2013

Agizo la Rais Kikwete la ahadi ya maji Magu laanza kutekelezwa.


Naibu Waziri  wa Maji Mh.  Binilith  Mahenge.
Na Immaculate Makilika- Dodoma
Serikali imemwajiri  Mtaalamu Mshauri  wa kusanifu miundombinu ya maji katika mji wa Magu,hatua hiyo ni  utekelezaji  wa agizo la  Rais  Jakaya  Kikwete la kutatua tatizo  sugu  la  maji  kwenye  eneo  hilo  mji wa  huo.
Naibu Waziri  wa Maji Mh.  Binilith  Mahenge alisema  hayo alipokuwa  akijibu swali la Dk. Festus Limbu Mbunge wa Magu –CCM  lililouliza ,je, Serikali haioni  kuwa haiwatendei haki  wananchi  wa mji  wa Magu  kwa kutotekeleza ahadi  hiyo  ya Mheshimiwa Rais.
Aidha Naibu huyo  alisema kuwa usanifu huo uliohuisisha miji midogo  ya Magu ,Nansio,Misungwi,Ngudu,Sengerema,Geita pamoja na jiji la Mwanza,na ulikamilika mwezi  Septemba   mwaka 2011.
Usanifu huo uligharimu   sh. bilioni 1.1 ambapo  gharama  ya ujenzi kwa mji wa Magu ilikadiriwa kuwa sh. bilioni 24.
Hata hivyo Serikali kwa kushirikiana  na wafadhili itagharamia ujenzi wa miradi  ya maji ya jiji la Mwanza ,miji ya Misungwi ,Magu ,Lamadi  na usafi wa mazingira kwa miji ya Bukoba na Musoma.
Benki ya Maendeleo  ya Ulaya (EB) na Shirika  la Maendeleo  la Ufaransa (AFD) watatoa jumla ya Euro  milioni  105 sawa  na sh. bilioni  214 kugharamia utekelezaji wa miradi  hiyo.
Kabla ya kuanza ujenzi ,wafadhili waliona wajiridhisha na gharama  zaujenzi  kwa kufanya mapitio  ya usanifu  uliofanyika awali na kujumuisha vijiji vilivyopo umbali wa kilometa 12 kutoka bomba kuu.
Wataalamu washauri wanaopendekezwa  kufanya mapitio  ya usanifu  wa miradi hiyo watawasilisha mapendekezo  yao ya kiufundi  na kifedha mwanzoni  mwa mwezi June  mwaka 2013,alisema Naibu Waziri huyo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...