| Kada wa CCM Ndugu Mtela Mwampamba akihutubia mamia ya wananchi kata ya Makuyuni wilayani Monduli kwenye kampeni za Uchaguzi wa Udiwani.Kada huyu wa CCM amewaomba wananchi wa MAKUYUNI ambao asiliyao kubwa ni kabila la Wamaasai kumchagua mgombea wa CCM kwenye uchaguzi utakao fanyika mapema tar.16/06/2013 siku ya jumapili.Amewasihi wananchi hao kuachana kabisa na siasa za chama cha upinzani kwa sababu vitawaletea vurugu,pia havina dira ya maendeelo.Nanukuu"Vyama vya siasa hasa hicho CHADEMA nashukuru hamkujitokeza kwenye mkutano wao wajana wakaishia kuondoka patupu,Nimekuwa chadema zaidi ya miaka 5 hakuna siku tuliyopanga kuleta maendeleo ndani ya nchi yetu,hivyo vyama ni maarufu kwa kulalamika tu."Hivyo chagueni diwani wa CCM kwamaslahi ya wananchi na jamii yenu. |
No comments:
Post a Comment