Monday 24 March 2014

RAIS KIKWETE HAJAINGILIA MCHAKATO WA KATIBA

jk5Na Magreth  Kinabo –Maelezo
Umoja wa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba la Tanzania Kwanza   wasema kwamba   Mhe. hotuba ya Rais,Jakaya Kikwete aliyoitoa wakati wa uzinduzi  wa Bunge Maalum   la Katiba  ,haikururuga wala kuingilia mchakato wa kupata Katiba Mpya ,bali  alitoa maoni na ushauri kama kiongozi wa nchi.
Aidha wajumbe hao wamesema Rais hakuingilia kanuni za bunge hilo zilizopitishwa, hakubadilisha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na hakupiga kura kwenye vifungu vya Katiba.
Kauli hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti  wa wajumbe hao, Said Nkumba katika mkutano na waandishi habari uliofanyika kwenye ukumbi wa waandishi wa habari wa Bunge mjini Dodoma.
 Nkumba ambaye aliambatana na  baadhi ya  wajumbe wengine watano , ambapo alisema  hotuba  hiyo  imeweka wazi faida na hasara za mifumo yote ya Muungano  wa Tanzania kwa hoja ili Watanzania wawe nnnnnna fursa pana ya kutafakari na kuamua
“ Rais ametimiza kauli yake ya kushawishi kwa hoja na si kulazimisha,” alisema Nkumba.
 Aliongeza kuwa alichokifanya Rais katika hotuba yake ni   kama kiongozi mkuu wan chi mwenye hekima na busara na uchungu wa nchi yake na  kutambua dhamana aliyopewa na Watanzania wote bila kujali makundi ameelezea faida na hasara za mifumo ya Serikali  iliyowasilishwa kwenye hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba.
“ Rais  katupa moyo na kutuhimiza tumalize kazi haraka na tuifanye kwa weledi huku tukiweka maslahi ya taifa mbele. Hata pale alipotoa maoni na ushauri kuhusu baadhi ya vifungu bado alisisitiza  kwamba umamuzi wa mwisho  ni wetu sisi wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba,” alisisitiza.
 Nkumba alifafanua kuwa  dhana ya kuichambua na kuikosoa Rasimu ya  Mabadiliko ya Katiba  si kumdhalilisha Mwenyekiti wa Tume na Wajumbe wake. Hivyo msingi mzima wa kutolewa rasimu hiyo ni kwamba wananchi waichambue, kuikosoa ,kuboresha  na kuirekebisha na hata ikibidi kuibadilisha na mwisho kuipigia kura.
 Alisema rasimu hiyo haikuletwa kama Msahafu wala Bibilia Na ndiyo maana zimewekwa hatua mbili  baada ya kazi ya tume kumalizika ,ambazo ni bunge hilo na kura ya maoni ya wananchi.
 Aliwataka wajumbe wa bunge hilo kushirikiana ili kuweza kuifanya kazi hiyo.
 Wajumbe wa bunge hilo wa Tanzania Kwanza wapo takribani 400 na watatoka katika makundi mbalimbali ,ambaomsimamo wao ni kushawishi kwa hoja na wala hawatalazimisha.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...